Hippo Parish Mjimwema Songea

Karibu katika tovuti ya kanisa Anglikana Dayosisi ya Ruvuma, mtaa wa mtakatifu Agustino Hippo Parishi Mjimwema Songea,kwa mawasiliano SLP 600 Songea ,baruapepe ni hippoparish.mjimwema@gmail.com

Thursday 9 March 2017

NIWAKARIBISHE KATIKA KIPINDI HIKI CHA KWARESMA,TUTUBU, NA KUONYESHA UNYENYEKEVYU VY

IBADA YA JUMAPILI TAR 07/08/2016
KANILA LA ANGLIKANA TANZANIA
DAYOSISI YA RUVUMA
KANISA LA MT. AGUSTINO-MTAA MJIMWEMA SONGEA
SOMO: REHEMA ZA MUNGU
MHUBIRI Mwl. PETER MAKWENDA
SEHEMU YA I
Utangulizi
Chukua mfano wa mwanafunzi aliyefanya kosa shuleni, halafu kama mwalimua au mzazi ukamchukua ukamhoji, je kwa nini umefanya hivi, atakuambia mwalimu (au mzee) mimi sijafanya hili na unajua kabisa aliyefanya jambo hili ni Simon( mfano), unamuambia Simon hebu niambie kwa hakika ni nani amefanya hili kama si wewe, atakuambia Baba unajua tulikuwa tunacheza tu, kwa bahati mbaya tukadondosha TV ikapasuka, au mwalimu sikuwa nimedhamiria kuumiza ila tulikuwa tunacheza nikamrushia kalamu ndio kwa bahati ikamchoma kwenye jicho, baada ya huyu mtu kufahamu kosa alilolifanya ataomba msamaha na akishapewa msamaha atapewa kazi ya kufanya, mwingine anaweza pewa eneo la kufyeka au kwa sababu umemuumiza mweza hautopewa pocket money kwa muda wa week 3 au kutohudhuria michezo kwa muda wa mwezi mmoja


Na baba yetu pamoja na mama yetu, Adama na mkewe Hawa walipofanya kosa walipewa msamaha lakini kuna jambo la kufanya walipewa wakaambiwa (Mwa 3:17) “... kwa jasho la uso wako utakula Chakula ....” Sasa ile adhabu inaposimama ndipo tunapoanza kutazama upande wa pili wa rehema.
Sasa je, Rehema ni kitu gani? Tunasema kwa lugha rahisi kwamba rehema ni ondoleo la adhabu baada ya kosa au inayoambata na kosa kupewa msamaha. Kosa linapofanyika linatanguliwa na msamaha halafu rehema ndipo inaposimama, kwa hiyo rehema inasimama kutuondolea adhabu baada ya sisi kusamehewa makosa yetu
. Ukisoma kitabu cha Kut 20:4-6 “ ... ni Mungu nwenye wivu, nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, name nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu”. Maandiko yanasema kosa linapofanyika halafu mtu asipotubu lile kosa, au msamaha unapotoka halafu lile lililotolewa msamaha halijafanyiwa, kazi basi kosa hilo linapatilizwa kwa wana hata kizazi cha tatu hata cha nne cha wote wenye kumchukia MUNGU
SEHEMU YA II
Sasa Je, rehema inakuja wapi? Rehema inakuja ili kusimamisha kule kupatilizwa kosa kwa ntoto hadi kizazi cha tatu na cha nne, ili kila mtu abebe mzigo wake MWENYEWE. Ezekiel 17:1-17 “... hatakufa huyu kwa sababu ya uovu wa baba yake, hakika ataishi” Kwa hiyo rehema inasimama baada ya mtu ( iwe baba au mama) amejua kosa anaumua kuomba rehema ili watoto wake wasipatilizwe, akasema nimeamua kumtafuta MUNGU, akishamtafuta tu REHEMA inaingia kwenye kizazi cha mwana, halafu kizazi cha tatu, cha nne na kuendelea “maelfu elfu” wampendao MUNGU, badala ya kupatilizwakosa kinaingia kitu kinachoitwa Baraka, kwa hiyo ili Baraka iendelee inabidi watu waendelee kumpenda YESU na kuzishika
amri zake. Kwa tunafahamu sasa kwamba rehema si ya bure, hatuwezi kupata rehema mpaka bure ila tutapata baada ya kuwa tumefanyaka kazi. Rehema ni tofauti kidogo na neema, ebu tuangalie kidogo, tunaposema neema tunamaanisha kustahilishwa kwa mtu asiyestahili, mwanzoni mimi, wewe na kila mmoja alikuwa ana kosa pamoja na asili ya kufanya dhambi. Kwa hiyo ile asili ya kufanya dhambi kila wakati ikwa inamvuta mtu aendelee kufanya dhambi. Anasema katika Yoh 3:16 “ Kwa maana jinsi hii MUNGU aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila amwaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele”
Kwa hiyo hatuhitaji kulipa (kitu) ili tupate neema, ila tunahitaji kazi ya kufanya ili rehema iingie, rehema ili iendelee kukaa tunatakiwa kufanya kitu. Neema inamuokoa mtu mmoja kwenye familia lakini rehema inaokoa kizazi ngoja nirudie tena hapa Neema inamuokoa mtu mmoja kwenye familia lakini rehema inaokoa kizazi hata kizazi, Yohana anaandika maneno ya YEsu anasema “... ili kila amwaminiye....” Maana yake ni kwamba baba anaweza kuwa anaamini lakini mama asiamini au baba anaweza kuwa anaamini lakini mwana asiamini na kwa hiyo baba ataokolewa kwa neema lakini sio mtoto kwa sababu baba ameokolewa. Lakini Rehema inapoingia Mungu anasema hivi , “ name nawarehemu maelfu elfu wanipendao na kuzishika amri zangu” kwa sabau gani kazi aliyoifanya baba inatembea mpaka kwa mtoto, leo tunao ujasiri kusema MUNGU wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka na MUNGU wa Yakobo kwa sababu ya kazi ya mtu mmoja Ibrahimu ambae alikubali kumtafuta MUNGU na ahadi zake,ndipo rehema za MUNGU kwa Ibrahimu zikatembea mpaka kwa watoto
Tunasoma Mazungumzo mazuri sana kati ya MUNGU na Sulemani katika 1 Fal 3;5-15, “ Sulemani akasema, umemfanyia mtumwa wako Daudi baba yangu fadhili kuu, kadiri alivyoenenda mbele zako katika kweli, na katika haki ....” Kwa hiyo MUNGU alimtokea Sulemani si kwa sababu ya Sulemani bali kwa sababu ya Daudi baba yake
Kwa hiyo tunaona tofauti kati ya neema inayookoa mtu mmoja na rehema inayookoa vizazi hata vizazi, ili kizazi kiekae katika Baraka basi unahitaji sana kukaa katika rehema, ebu tusome kidog Rum8:1 “ sasa basi hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika KRISTO YESU” Kwa hiyo rehema inakuja kusimama badal aya hukumu ya adhabu
Nini tunahitaji ili kusiimamisha Baraka katika vizazi
Rehema si bure bali inahitaji tufanye kazi ili rehema itembee katika vizazi vyetu. Mambo yafuatayo ni msingi wa kusimamisha rehema katika vizazi
(i) Yoh 3:16, Yoh 1:12 Kumwamini YESU, huku kunamsogeza mtu na kizazi chake
katika rehema za MUNGU (ii) Yoh 14;15 “ Mkinipenda mtazishika amri zangu” Jambo la pili ni kumpenda
MUNGU na kushika amri zake (iii) Rum 8:1, “sasa basi hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika KRISTO YESU” kukaa ndani ya YESU, kwa YESU ndiko kwenye rehema kwa hiyo ili kukaa kwenye rehema mtu anahitaji kukaa ndani ya YESU
Na hizi ndizo faida za MTU kukaa na REHEMA za MUNGU
(a) Kuondolewa laana za vizazi, Kut 20: 4-6, (b) Kufanikiwa na kuinuliwa Zab 27;4, 23:6 (c) Kuheshiwa mbele za watu na mbele za MUNGU, Yoh 12: 26
Tamani sana Kukaa na Rehema za Mungu ili kusimamisha Baraka katika vizazi vyako na kuona mkono wa MUNGU ukizidi kutembea na wewe, milele yote
MUNGU Mwaminifu, mshika maagano azidi kukubariki
Mwl. Peter Makwenda
+255 754 615213
makwendap@gmail.com

No comments:

Post a Comment